Translate

Tuesday, April 8, 2014

VOICE OF TRUIMPH...........WE SPEAK LIFE



Ikiwa chini ya vijana wenye damu changa, wanaotafuta kumfahamu Kristo na Kumtumikia, VOICE OF TRIUMPH (VoT), walianza rasmi tarehe 8 mwezi wa 4, 2012 ndani ya community Church ikiwa mara yao ya kwanza kabisa kuwasilisha wazo lao miongoni mwa watu waliokuwa na shauku kuona mwamko mpya wa muziki wa dini mkoani ARUSHA. 




 

   Tolla G Tolla, kama raisi wa VOT alionesha  maono ya kikundi hiki na kuamsha hamasa miongoni mwa wajumbe waliohudhuria…wakiwa bado wachangaaaaa…waliimba baadhi ya nyimbo zilizo kosha mioyo ya wengi na kuamsha mshawasha wa kuwasikia tena. 

 

    Leo ni miaka kama 2 sasa tangu kuanzishwa kwa kundi hili. Tayari yamefanyika mengi na kukua kwa kundi hili kwaonekana bayana.

   Siri kubwa ya mafanikio haya ni kule kujitoa pasi na mwisho kwa waimbaji na wajumbe wa kikundi ndo kunako pelekea kuona maono yao ya mwaka 2010…..yakionekana wazi.

    Ni dhahiri kuwa Mungu anapotoa maono anayatoa kwa watu walio tayari, kufanya, wapo waliokuwa mstari wa mbele lakini leo hawapo, wapo walioona wakasadiki na kujiunga na wapo waliokuwa na imani wakaona yakitokea wakiwepo. Sifa na SHUKRANI ZIMWENDEE MUNGU.

    Ni ukweli kwamba wanamuziki wengi wa nyimbo za injili nchini Tanzania hawana umoja huu ulioanza kwa VOT, hivyo mwamko huu uombewe na kupewa msaada wa kifedha na kihali kufanya kazi ya  Bwana Yesu iende mbele.


 
Ni maombi yangu kuwa VOT wafanikiwe kila wakati….


No comments:

Post a Comment