Translate

Tuesday, November 22, 2016


Je ni kweli kuwa Mungu huwapatiliza wana DHAMBI za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne?
Baadhi ya maandiko yanakubaliana na kauli hii, kuwa dhambi za baba huamishiwa kwa watoto wao. Lakini ni vema tukatulia kidogo na kuangalia uhalisia wa maneno haya, na maandiko mengine yanayotilia msisitizo ama kukinzana na andiko hili.
Kwa upande mmoja inaonekana ni kweli Mungu huwapatiliza wana maovu ya baba zao.
Kutoka 34:6-7
“BWANA akapita mbele yake akatangaza, BWANA, BWANA, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; wenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne”
Kumbukumbu 5:8-10
‘Usijifanyie sanamu ya kuchong, mfono wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, au kilicho chini duniani , au kilicho majini chini ya nchi.  Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi ni BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, nawapatiliza wana uovu wa baba zao; hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu’
 Walawi 26:39
“Na watu wa kwenu watakaobaki watafifia kwa ajili ya uovu wao, katika hizo nchi za adui zenu; tne watafifia kwa ajili ya uovu wa baba zao, pamoja nawo"

 Kwa upande mwingine maandiko yanaonekana kukinzana na maandiko hayo mawili. Lakini sio kweli kwamba yanakinzana.
Kumbukumbu 24:16
Mababa wasiuawe kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya baba zao; kila mtu na auawe kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe,”
 2 Wafalme 14:6
Ila hakuwaua watoto wa hao wauaji; kama ilivyoandikwa katika kitabu cha torati ya Musa, kama alivyoamuru BWANA, akisema, mababa wasife kwa makosa ya wana , wala wana wasife kwa makosa ya mababa; lakini kila mtu atakufa kwa kosa lake mwenyewe.“
Ezekia 18:20
“Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake na uovu wake menye uovu utakuwa juu yake.”

Je maandiko haya yanamahusiano gani?
Kwa jinsi Mungu alivyo na tabia zake haya maandiko yanamahusiano makubwa. Kwanza; dhambi ya baba anaadhibiwa nayo mtoto ….hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao….kama wana hawajamjua Kristo na kuunganishwa na agano la Kristo ni dhahiri kuwa dhambi za baba zao zitaambatana nao.
Tabia moja wapo ya Mungu ni kuwa ni wa haki…kwa mantiki hiyo Mungu huwaadhibu walio na makosa na sio wale waliotubia makosa yao.
Pili; kwa sababu ya Kristo laana zote za aina zote Yesu alizibeba msalabani . kwa mantiki hiyo kila aziungamae dhambi zake kweli anasamehewa na anakuwa kiumbe kipya.
2 Kor 5: 17
Hata imekuwa mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kumbe kipya; yakale yamepita tazama yamekuwa mapya”
1 Yoh 1:9

Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. 


No comments:

Post a Comment