Translate

Thursday, August 4, 2016



<![endif]-->
Je kunena kwa lugha hutoka kwa Mungu ama Kwa shetanI?
Kitu cha muhimu cha kufahamu kuhusu kunena kwa lugha ni alichokisema Yesu kuhusu kunena kwa Lugha. Marko 16:17
“Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;…..”
Bwana Yesu, alishuhudia kuwa kunena kwa lugha ni alama ya nguvu ya Mungu kwa hao waaminio. Mungu hakuwapa Watoto wake karama zilizo mbaya; kwa mantiki hiyo hatuogopi ama kuikashifu karama yeyote ya Roho Mtakatifu ikiwemo kunena kwa Lugha.
Watu wengine wanasema, wakristo walio wengi hunena kwa kuigiza kwa watu wengine. Hilo linabaki kuwa siri ya anenaye na Mungu wake. Ila anenaye na kwa Lugha anazo faida nyingi. Inamsaidia kuwasiliana moja kwa moja na Mungu.
Kulingana na mtume Paulo, katika 1 kor 13:1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo , nimekuwa kama shaba iliayo na upatu uvumao.”

Unapopokea karama ya kunena kwa lugha Roho Mtakatifu anadownload lugha na kuhifadhi kwenye roho yako bila wewe kuisoma hiyo lugha. Niseme wazi kuwa ni Lugha na sio kaneno kanakojirudia rudia manake huwezi kuomba ama kuongea na Mungu kwa neon moja.
Mwaka 2006, Dr. Andrew Newberg wa chuo kikuu cha Pennsylvania alichukua picha za ubongo za watu watano waliokuwa wakinena kwa lugha, baada ya utafiti wake alisema, “ tumeona mabadiliko makubwa kwenye uwezo wa kufanya kazi wa ubongo na kugundua kutokuwepo uwezo wa binafsi wa ubongo wa kufanya kazi, hii inaonyesha uwezo wa ziada wa kuzungumza bila mzungumzaji kujitambua…hili ni jambo la ajabu” alisema. Hii ina maana kuwa kunena kwa lugha ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

1.      Je kunena kwa lugha ni zawadi maalumu kwa watu maalumu?
Kunena kwa lugha imeonekana sana kama karama ya Roho mtakatifu katika agano Jipya. Katika Mdo 2:4, biblia inasema kuwa wanafunzi wa mwanzo 120 walinena kwa Lugha katika chumba cha juu; “wote walijazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa Lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka”
Hatujui kama wote walipokea kipawa cha Imani ama kuponya ama kutoa pepo, lakini tunajua kwa hakika kuwa walinena kwa lugha mpya kama Roho alivyowajalia.
Leo kuna wakristo waongofu wengi sana duniani, na wanaomwamwini Kristo, na wanatengeneza kundi kubwa linalokuwa kwa haraka sana duniani. Karama ya kunena kwa LUGHA sio ya kundi dogo lililochaguliwa na Roho Mtakatifu bali ni kwa wote wanaomwamini Bwana Yesu na wanao amini kazi za Roho Mtakatifu. Mtume Paulo amelisema wazi katika 1Kor 14:5 kuwa “Nami nataka ninyi nyote mnene kwa Lugha, lakini Zaidi sana mpate kuhutubu, maana yeye ahutubuye ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha, isipokuwa afasiri, ili kusudi kanisa lipate kujengwa”
Kwa mantiki hii Matume Paulo anatamani kila mtu anene kwa lugha kwa ajili ya kujijenga kiroho Zaidi na kuhutubu kwa ajili ya kulijenga kanisa.
2.   Je karama hii iliisha baada ya karne ya kwanza ama hadi sasa inafanya kazi?
Kuna baadhi ya wasomi wa Dini wanao amini kuwa karama za Roho Mtakatifu ziliishia karne ya kwanza (the doctrine of cessationism). Kwenye andiko hili wanaamini kuwa karama zote za roho mtakatifu ziliisha baada ya wanafunzi 12 kufariki. Lakini kuna maandiko ya mababa wa Imani kama Justin Martyr (100-165), Irenaeus (115-202), Turtullian (160 -220) na Origen (185 -254) wanashuhudia kuwepo kwa karama hizi ikiwemo kunena kwa Lugha wakati wakihudumu katika kanisa enzi zao muda mrefu baada ya Mtume Yohana kufariki miaka 100 baada ya Kristo.
Mtume Petro anashuhudia katika Mdo 2:39 kuwa karama ya kunena kwa lugha ni kwa wote walioitwa na Mungu; “kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa wote walio mbali na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”
Mtume Paulo pia anaandika katika 1kor 13:8,9 kuwa ile iliyokamili itakapokuaja, kunena kwa lugha kutakoma. Hii ni ina maana atakapokuja Kristo (iliyo kamili) kwa mara ya pili ndipo karama hii na nyinginezo zitakoma. Maana biblia inafundisha kuwa hakuna aliye mkamilifu ila mmoja ndiye Yesu. Atakapokuja hatutakuwa na haja ya kunena kwa lugha kuwasiliana na Mungu kwa maana tutakuwa naye. Kwa mantiki hii karama ya kunena kwa lugha ipo kwa kila mwamini anayetaka kuipokea.
3.   Watu husema nini wanaponena kwa Lugha?
Biblia inafundisha mambo matano makuu matano mtu anapoomba kwa lugha:
a)      Anawasiliana moja kwa moja na Mungu.
1Kor14:2 “maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna askikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake.”
Kunena kwa lugha ni njia ya moja kwa moja ya kuwasiliana na Mungu.
b)     Wanasifu matendo makuu ya Mungu
Katika Mdo 2:11, “……; tumewasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu”
Mbali na kuwa ni ujinga (kama wengine wasemavyo) kunena kwa lugha kunamtukuza Mungu na matendo yake makuu kwetu. Hii inawezaje kuwa jambo baya?
c)      Wanamwadhimisha Mungu.
Katika Mdo 10:46, “kwa maana waliwaskika wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu….”
Hata kama hatuelewi tunachosema tunaposema kwa Lugha tunajua kuwa tunamwadhimisha Mungu katika Roho (1kor 14:16)
d)     Wana jijenga wenyewe kiroho
Mtume Paulo anasema katika 1Kor 14:4, “Yeye anenaye kwa lugha hujijenga nafsi yake; bali ahutubuye hulijenga kanisa.”
Kunena kwa lugha ni kama karakana ya kiroho, unajijenga kiroho na kuwa imara pia kiroho.
e)      Roho Mtakatifu anasali ndani yao.
Katika kitabu cha Warumi 8:26,27, “ …….kw maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa……kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.
Kuomba kwa Roho huleta ufunuo na maono ya mapenzi ya Mungu kwako. Hivyo kunena kwa Lugha ni kiungo muhimu cha kuombewa na Roho mtakatifu.
Kama hauna Imani juu ya karama ya kunena kwa lugha ama ulishakuwa na mtazamo hasi kuhusu karama hizi nakutia moyo kusoma biblia na kuomba ufunuo wa kimaandiko kuelewa. Mwombe Roho Mtakatifu akufunulie ukweli kuhusu karama hii.
Wako pia watu wengi waongofu, wanaotamani kunena kwa lugha, kwa bahati mbaya badala ya kutulia na kumwomba Mungu wanaiga unenaji wa watu wengine ili tu waonekane nao wananena kwa lugha. Hii sio nia ya Roho mtakatifu na ni dhambi kudanganya nafsi yako na wanaokuzunguka.
Kama nlivyotangulia kusema, lugha inakua vivyo hivyo na lugha ya Roho Mtakatifu, unaponena mara kwa mara Mungu anakuongezea misamiati na unakuwa na upeo mpana wa kuongea Lugha ya Roho Mtakatifu.
Yesu anasema katika Luka 11:13, “ basi ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao”?
Wakati mwingine twatakiwa kuomba na kuzidi kuomba mpaka tutakapo pokea tukiombacho. Kama umevuviwa tayari karama yoyote itumie kila wakati ili izidi kufanya kazi ndani yako. 1Kor14:18, Paulo anajisifu kuwa; “Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha Zaidi ya ninyi nyote”
Je kuna matumizi yasiyo sahihi ya karama ya kunena kwa lugha?
Ndiyo, bila shaka kuna watu hunena kwa lugha bila utaratibu na kwa matumizi ya tamaa zao wenyewe na wanahitaji kuelekezwa na kufundishwa. Lakini usimtupe jongoo na mti wake kwa kukataa kuwepo kwa karama ya kunena kwa lugha kwa ajili ya matumizi mabaya ya hii karama. Tujifunze kwa mtume Paulo anaposema katika 1Kor 14:39, “kwa ajili ya hayo, ndugu, takeni sana kuhutubu, wala msizuie kunena kwa lugha.




No comments:

Post a Comment